Zodiaki ni kanda kwenye anga zenye upana wa takriban nyuzi 20 zinazofuata mstari wa njia ya Jua yaani mstari wa njia dhahiri ya Jua angani katika mwendo wa mwaka mmoja. Mstari huo unapatikana kwa kutazama Jua wakati wa mapambazuko ambako linaonekana katika mazingira ya makundinyota tofauti. Kila mwaka Jua linapambazuka katika eneo la makundinyota yaleyale.

Zodiaki angani, mchoro wa mwaka 1442 katika kuba ya kanisa la Italia, ikionyesha mstari wa njia ya Jua kati ya makundinyota ya ekliptiki.

Njia dhahiri za Mwezi na sayari zinaonekana pia katika kanda hii ya zodiaki.

Hadi leo unajimu unatumia makundinyota 12 kama buruji za falaki kwa imani ya kwamba nyota hizi zina athari kwa kipindi fulani cha mwaka kinachoitwa kufuatana na kundinyota au buruji ya falaki yake. Lakini hali halisi Jua linapita katika maeneo ya makundinyota 13, si 12.

Miaka 3000 iliyopita, ambapo mfumo wa Zodiaki ulibuniwa, wataalamu wa Babeli waliondoa kundinyota la Hawaa (Ophiuchus) katika mfumo kwa shabaha ya kupata mgawanyo wa anga unaolingana na miezi 12 ya kalenda.

Kumetokea pia badiliko la kwamba makundinyota ya Zodiaki hayalingani tena na vipindi vya mwaka ambapo yanatangazwa na wanajimu wa leo. Sababu yake ni kusogea kwa mhimili wa Dunia na hii inasababisha ya kwamba sisi tunatazama anga kwa pembe tofauti kuliko wazee miaka 2000 iliyopita. Ila tu wanajimu wanaendelea kutumia vipindi vilivyopimwa zamani zile.

Makundinyota ya ekliptiki hariri

Jedwali lifuatalo linaonyesha hali halisi ya makundinyota 13 yanayopitiwa na Jua katika mwendo wa mwaka mmoja. Kwa sasa nukta ya machipuo iko ndani ya Hutu (Pisces) hivyo hapa iko nafasi ya 0°

KundinyotaIsharaNafasi kwenye
ekliptiki
Kipindi cha kupita
kwa Jua (mwaka 2010)
Kipindi cha Buruji ya Falaki
inayolingana katika unajimu
KiswahiliKilatini
Kondoo (Hamali)Aries 28,8°–53,5°19. Apr – 14. Mei21 Machi- 19 Aprili
Ng'ombe (Tauri)Taurus 53,5°–90,2°14 Mei – 21 Juni20 Aprili – 21 Mei
Mapacha (Jauza)Gemini 90,2°–118,1°21 Juni– 20. Julai22 Mei – 20 Juni
Kaa (Saratani)Cancer 118,1°–138,2°20 Julai – 11. Agosti21 Juni – 22 Julai
Simba (Asadi)Leo 138,2°–173,9°11 Agosti – 17. Sept23 Julai – 22 Agosti
Mashuke (Nadhifa)Virgo 173,9°–218,0°17 Sept – 31 Okt23 Agosti – 22 Sept
MizaniLibra 218,0°–241,0°31 Okt – 23 Nov23 Sept – 23 Okt
Nge (Akarabu)Scorpius 241,0°–247,7°23 Nov – 30 Nov24 Okt – 21 Nov
HawaaOphiuchus 247,7°–266,3°30 Nov – 18 Des(ilipunguzwa katika unajimu)
Mshale (Kausi)Sagittarius 266,3°–299,7°18 Des – 20 Jan22 Nov – 21 Des
Mbuzi (Jadi)Capricornus 299,7°–327,6°20 Jan – 16 Feb22 Des – 19 Jan
Ndoo (Dalu) Aquarius 327,6°–351,6°16 Feb – 12 Machi20 Jan – 18 Feb
Samaki (Hutu)Pisces 351,6°–28,8°12 Machi – 19 Apr19 Feb – 20 Machi

Tazama pia hariri

Makala hii kuhusu eneo fulani bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu eneo hilo kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Je, unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.


Usitaje majina ya madiwani na viongozi au maafisa wengine wa sasa maana wanabadilika haraka mno.

Makundinyota ya Zodiaki
Majina ya kisasa yanafuatwa kwa mabano na jina la mabaharia na jina la Kilatini (la kimataifa)

Kaa (Saratani – Cancer )Kondoo (Hamali – Aries )Mapacha (Jauza – Gemini )Mashuke (Nadhifa – Virgo )Mbuzi (Jadi – Capricornus )MizaniLibra ) • Mshale (Kausi – Sagittarius )Ndoo (Dalu – Aquarius )Nge (Akarabu – Scorpius )Ng'ombe (Tauri – Taurus )Samaki (Hutu – Pisces )Simba (Asadi – Leo )