Libya ni nchi ya Afrika ya Kaskazini kwenye Bahari ya Mediteraneo, inayopakana na Misri, Sudan, Niger, Chad, Algeria na Tunisia.

ليبيا
(Lībiyya)
Libya
Bendera ya Libya
Nembo la Libya
Lugha rasmiKiarabu
Mji MkuuTripoli
SerikaliJamhuri ya Kiislamu
Mkuu wa DolaMohamed al-Menfi
Waziri MkuuAbdul Hamid Dbeibeh
Eneokm² 1.759.541
Idadi ya Wakazi7,054,493 (Julai 2022)
Wakazi kwa km²3,74
JPT/mkazi4.293 US-$ (2004)
Uhurukutoka Italia tarehe 24 Desemba 1951
PesaDinari ya Libya
WakatiUTC+1
Wimbo la Taifa"Libya, Libya, Libya"
Mahali pa Libya katika Afrika
Ramani ya Libya
Ziwa la Um el Maa huko Libya

Eneo kubwa la nchi (90%) ni sehemu ya jangwa la Sahara. Chini yake kuna akiba kubwa ya petroli, ambayo ndiyo utajiri wa nchi.

Miji mikuu ni Tripoli, Benghazi na Misratah.

Historia hariri

Wakazi asili walikuwa Waberber. Baadaye wakaja Wafoinike upande wa magharibi na Wagiriki upande wa mashariki.

Hatimaye Libya ikamezwa na Dola la Roma, na Ukristo ukaenea.

Baada ya dola hilo kuanguka, Wavandali waliteka sehemu kubwa ya nchi.

Katika karne ya 7 Waarabu waliingiza Uislamu na utamaduni wao.

Mwaka 1551 Waturuki walifukuza Wazungu kutoka Tripoli wakatawala hadi karne ya 20.

Nchi ilitawaliwa na Waitalia tangu mwaka 1911 hadi 1941 ilipotekwa na Waingereza ambao, baada ya Vita vikuu vya pili kwisha, waliacha nchi mwaka 1951 mikononi mwa mfalme mwenyeji, Idris I, aliyekuwa amepinga ukoloni tangu mwaka 1920 (Vita vya Libya dhidi ya Italia).

Kisha kumpindua mfalme huyo, Muammar al-Gaddafi alitawala kidikteta tangu mwaka 1969 hadi alipopinduliwa na kuuawa mwaka 2011 kwa mkono wa N.A.T.O.

Baada ya hapo wananchi wanazidi kupigana katika vita vya wenyewe kwa wenyewe. Mwaka 2020 kulikuwa na makubaliano ya kusimamisha vita na kuunda serikali ya pamoja ili kuandaa uchaguzi mkuu.

Watu hariri

Wakazi wa Libya ni hasa mchanganyiko wa Waberberi, Waarabu na Waturuki (74%), mbali na Waberberi (25%) ambao ndio wakazi asilia, lakini wengi wao wameanza kutumia lugha ya Kiarabu pia. Kuna pia wahamiaji kutoka nchi za jirani, za kandokando ya Bahari ya Kati na kutoka Bara Hindi.

Wakazi wameongezeka tangu mwaka 1970 kutoka milioni 2.5 hadi kuwa karibu milioni 7 mwaka 2022. Nusu ya wakazi wote ni vijana chini ya umri wa miaka 16. Sehemu kubwa kabisa (80%) huishi sehemu za pwani.

Lugha kuu ni Kiarabu pamoja na lugha kadhaa za Kiberberi.Ndizo:

Upande wa dini, unatawala Uislamu (97%). Wakristo ni zaidi ya 100,000, wakiwemo hasa Wakopti (60,000) na Wakatoliki (40,000).

Tazama pia hariri

Viungo vya nje hariri

WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:


Nchi za Afrika
Afrika ya Kati (Jamhuri ya) | Afrika Kusini | Algeria | Angola | Benin | Botswana | Burkina Faso | Burundi | Cabo Verde | Chad | Cote d'Ivoire | Eritrea | Eswatini | Ethiopia | Gabon | Gambia | Ghana | Guinea | Guinea Bisau | Guinea ya Ikweta | Jibuti | Kamerun | Kenya | Komori | Kongo (Jamhuri ya) | Kongo (Jamhuri ya Kidemokrasia ya) | Lesotho | Liberia | Libya | Madagaska | Malawi | Mali | Misri | Morisi (Visiwa vya) | Mauritania | Moroko | Msumbiji | Namibia | Niger | Nigeria | Rwanda | Sahara ya Magharibi | Sao Tome na Principe | Senegal | Shelisheli | Sierra Leone | Somalia | Sudan | Sudan Kusini | Tanzania | Togo | Tunisia | Uganda | Zambia | Zimbabwe
Maeneo ya Afrika ambayo ni sehemu za nchi nje ya Afrika
Hispania: Kanari · Ceuta · Melilla | Italia: Pantelleria · Pelagie | Ufaransa: Mayotte · Réunion | Uingereza: · St. Helena · Diego Garcia | Ureno: Madeira
Makala hii kuhusu maeneo ya Afrika bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Libya kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.